TGNP Publications
KUFANYA MABADILIKO: Vibonzo
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kwa kushirkiana na shirika la kimataifa la watu wa Canada (GAC) kupitia shirika la SeedChange lililopo nchini Canada, tunatekeleza mradi wa pamoja ujulikanano kama “Wanawake wa Vijijini Waleta Mabadiliko—Rural Women Cultivating Change (RWCC)”.
Kitabu hiki cha katuni au maarufu kama Vibonzo kimetengenezwa kutoa njia rafiki kwa watu kutafakari, kufikiri, na kujadili baadhi ya masuala muhimu katika jamii ya Tanzania. Kupitia mchakato wa ushirikishwaji, waaandaaji wa kitabu hiki walitaka kuonesha, kwa kutumia katuni na hadithi rahisi, uhusiano kati ya unyanyasaji wa kijinsia, kilimo cha ikolojia, na ushiriki wa wanawake katika uongozi na maamuzi. Tunatumaini kuwa kwa kusoma kitabu hiki pamoja, wanajamii, hasa vijana wa vijijini, watajifunza njia ya kupaza sauti zao na kuwa vinara wa kuleta mabadiliko.
Wanafanya maamuzi pia wanaweza kujifunza mengi kuhusu kilimo cha ikolojia na njia zinazoweza kusaidia kilimo kama njia ya kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili wakulima, wanawake vijana, watu wanaoishi na ulemavu, na makundi mengine yaliiyopembezoni katika maeneo ya vijijini–-na kusaidia kuwawezesha kiuchumi.